Skip to main content

Jifunze kutype kwenye kompyuta bila kuangalia keyboard

Je unataka kuongeza ufanisi katika kazi zako za kompyuta? Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutype(kuandika) haraka haraka katika keyboard ya kompyuta bila kuangalia.

Kutype haraka katika kompyuta ni ujuzi ambao kila mtu anaweza kujifunza japo wengi hudhani wataalamu wa kompyuta ndio wanafanya mambo hayo. Ni ujuzi rahisi sana kama mtu ni mwenye bidii hata ndani ya mwezi unaweza kujifunza.

Kuna usemi usemao mti wa kudakia samaki (fishing rod) ni mwendelezo wa mkono wa mvuvi, kwa maana mvuvi mahiri anaweza kuhisi pindi samaki anapokuwa maaneo ya mti wake. Kama fishing rod ilivyo kwa mvuvi, keyboard ya kompyuta inabidi iwe mwendelezo wa vidole vyako ili uwe mtumiaji wa kompyuta mzuri.

Katika keyboard ya kompyuta kila kidole kina sehemu yake na kina sehemu kinaweza kwenda. Kujifunza kutype ni kujifunza namna ya kutumia vidole vyako inavyotakiwa. Katika kutype jambo kubwa la kuepuka ni kuinua mkono ili kufuata kitufe fulani, bila shaka kuna wakati utahitaji kuinua mkono lakini hii hutokea mara chache, kama vile ukitaka kutype namba zilizopo kwenye number pad.

Mambo ya kuzingatia wakati wa kutype

  1. Hakikisha umekaa vizuri na mikono yako ipo comfortable, hii itarahisisha kusogeza vidole na mikono kirahisi pindi inapohitajika.
  2. Vidole vyako vina sehemu maalumu ya kukaa ambayo ni ASDF kwa mkono wa kushoto na JKL; kwa mkono wa kulia. Vidole gumba unaviacha hauviweki kwenye hizi herufi. Huu mstari huitwa HOME ROW, yaani hapa ndio NYUMBANI ikitokea umehamisha kidole kwenda kubonyeza sehemu ingine inabidi ukirudishe NYUMBANI baada ya kumaliza.
  3. Kwenye herufi F na J utaona kuna kama kauvimbe fulani, hii inasaidia kuweza kurudi kwenye HOME ROW bila kuangalia keyboard.
  4. Usiangalie keyboard wakati wa kuandika, kumbuka lengo ni mazoezi ya vidole ili ubongo wako uzoee kufanya hivyo.
  5. Kila kidole kina vitufe ambavyo kinaruhusiwa kubonyeza, hivyo usitumie kidole tofauti. Pia kumbuka kurudi kwenye HOME ROW baada ya kubonyeza kitufe fulani.

Software au Programu za kujifunzia kutype

Tumeona namna kutype bila kuangalia kunavyofanya kazi, lakini ili kufanya mazoezi vizuri kuna programu nyingi za kompyuta zinazofundisha kutype.

Uzuri wa programu hizi zinapima spidi yako na uwezo wako wa kutype bila kukosea kadri unavyofanya mazoezi.

Pia programu hizi zinakua zinafundisha kwa mtindo wa games, labda ukitype haraka unapata marks fulani na kadhalika. Programu mojawapo yenye mtindo huu ni ile ya Typing Master.

Baadhi ya programu za kujifunzia kutype

  1. Typing Master (Maarufu)
  2. Kiran’s Typing Tutor (BURE)
Zingatia:

Ni bora kutype taratibu bila kukosea kuliko kutype haraka na makosa, kwa hiyo wakati unajifunza lengo kubwa jifunze namna ya kutumia vidole vyako na kuandika bila kukosea. Spidi ya kutype itakuja taratibu ukishaelewa matumizi sahihi ya vidole.

Hitimisho

Ni vizuri kutumia programu kujifunzia kutype, vile vile ni vyema kujitengea muda kila siku hata kama ni nusu saa kwa siku, kwani kutype ni kama mazoezi ukiyaacha unasahau, ukiyafanya kila mara unakua mjuzi zaidi.

Comments

  1. It is useful to me, and I wish if I would get your contacts.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Jinsi ya kuangalia faini za makosa ya barabarani Tanzania

Je ungependa kufahamu namna ya kucheck kama gari yako inadaiwa au haidaiwi? Unaweza kupata taarifa hizi kwa kutumia mtandao kwa wale wenye simu za internet, vile vile unaweza kutumia simu ya kawaida isiyo na internet. Kwa njia ya mtandao Kwa kutumia mtandao tembelea link ifuatayo. http://tms.tpf.go.tz Ukurasa ukifunguka ingiza namba ya gari lako, hapo utaona faini zilizopo katika gari lako. Pia unaweza kuchagua kuingiza namba ya leseni, ili upate faini zilizoandikwa katika leseni yako. Kwa njia ya simu Kwa kutumia simu ya kawaida piga *152*75#  , kisha fuata maelekezo, ukishamaliza utatumiwa ujumbe mfupi wenye taarifa za faini.

Fahamu file aina ya zip na jinsi ya kulitumia

Umewahi kudownload file kwenye internet na kukuta hilo file ni zip na ukashindwa kulifungua? Au umepokea barua pepe ndani yake kumeambatanishwa na file la zip? Au una file kubwa la game au software nyingine unataka kuliweka kwenye DVD lakini halitoshi kwenye hiyo DVD? Katika makala hii tutaangalia kwa undani file la zip (kifurushi) na matumizi yake mbali mbali. File la zip ni nini? File la zip ni file ambalo linakusanya mafile mengine na kuyaweka katika file moja. Hii huwa inarahisa kazi tofauti mfano kutuma barua pepe, badala ya kutuma mafile 10 yaliyomo kwenye folder moja, unaweza kutengeneza zip file moja na kulituma. Pia zip file husaidia kupunguza size ya file. Mfano mzuri wa mafile ambayo hupungua size maradufu ni mafile ya maandishi(text). Mafile ya picha, sauti au video mara nyingi hayapungui size sana kwa sababu aina za hayo mafile tayari yalishajaribu kuyapunguza size. Naandaa vipi file la zip? Ni rahisi sana kutengeneza file la zip, kwani utengenezaji wa file la zi