Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2018

Programu rahisi ya C: kujumlisha namba mbili

Je unataka kujua namna ya kufanya mahesabu katika programu? Programu yetu ya sasa itaonyesha namna ya kujumlisha namba mbili ambazo mtumiaji atakuwa ameingiza kwa kuandika na keyboard yake. Kama tulivyojifunza hapo awali kuwa stdio.h ni “Standard Input/Output header”, ambalo ni file lenye functions zinazohusiana na input(kuingiza) au output kama vile printf, kwenye somo hili tutajifunza function mpya ya scanf. Kazi ya scanf ni kuchukua/kusoma alichoandika mtumiaji kwa keyboard na kukihifadhi katika kompyuta kwa matumizi ya baadae kwenye programu. Programu ifuatayo inaonyesha kujumlisha tarakimu mbili #include <stdio.h> /* function main - Hapa ndipo programu inapoanzia kufanya kazi */ int main(void) { int namba1; /* namba ya kwanza itakayoingizwa */ int namba2; /* namba ya pili itakayoingizwa */ int jumla; /* variable itakayohifadhi jumla */ printf("Andika namba ya kwanza\n"); /* julisha kuwa namba inatakiwa kuingizwa */ scanf("%d"

Programu rahisi ya C: kuandika maandishi kwenye screen

Je unataka kuona jinsi programu ya C inavyoandikwa? Katika somo hili tutajifunza machache katika C, kadri tunavyoendelea kujifunza ntaongeza vitu mbali mbali kidogo kidogo, ili na wewe uweze kutafuna uliyojifunza! 1. Kuandika maandishi kwenye screen Programu ifuatayo itakuonyesha namna ya kuandika maandishi kwenye screen #include <stdio.h> /* function main - Hapa ndipo programu inapoanzia kufanya kazi */ int main(void) { printf("Karibu C Programu!\n"); return 0; /* Programu imemalizika bila tatizo */ } /* Mwisho wa main */ Output Karibu C Programu! 1.0. #include <stdio.h> Hii inaiambia C Preprocessor kuweka yaliyomo katika file la stdio.h kwenye hii programu. File la stdio.h yaani standard input/output header lina maelezo ambayo yanasaidia COMPILER kucompile programu yako kama umetumia function zilizomo humo. Kwa mfano printf ni moja ya function ambazo zipo kwenye stdio.h, kuna zingine nyingi tutaendelea kujifunza. function ni kipan

Jinsi ya kujifunza lugha ya kuprogramu ya C

Je unataka kuwa mtaalamu wa kutengeneza programu za kompyuta? unataka kufahamu njia ya kutimiza lengo lako kirahisi? Waswahili wanasema "Mtaka cha uvunguni sharti ainame" basi ndivyo hivyo hivyo ili kuwa mtaalamu wa kuprogramu inabidi uwe unaandika programu. Ujuzi wowote unaushika vizuri zaidi ukiwa ni mtendaji. Utajifunza mengi sana kwa kuandika programu zaidi ya kusoma C kwenye vitabu na mtandaoni. Hivyo weka bidii kufanya mazoezi tofauti tofauti ya kuprogramu iwe kwenye vitabu au kutengeneza programu ya suluhisho ya matatizo uliyoyaona mtaani, kwenye biashara au sehemu nyingine. Pia wakati unafanya mazoezi haya jitahidi kufuata miongozo ya kuandika programu nzuri yaani GOOD PROGRAMMING GUIDELINES. Kwenye programu zako hakikisha zinasomeka vizuri kwa maana nafasi kati ya maneno au mistari iwe ya kutosha. Pia jitahidi kuweka maoni (COMMENTS) ili iwe rahisi wewe kuelewa au mtu mwingine kuelewa programu yako. Ni kawaida kwa programmer kusahau sehemu flani ya programu yake

Historia fupi ya C

Je unataka kujua C ilitokea wapi? na kipindi gani? Lugha ya kuandikia programu za kompyuta ya C ilianzishwa mnamo mwaka 1970 na mbunifu wake Dennis Ritchie. Aliita C kwa sababu kipindi hicho alikuwa akitumia lugha iitwayo B katika kazi zake, hivyo C ilifuata baada ya B. Mbunifu wa C alichukua mazuri ya B na kuyaweka kwenye C, vile vile akaongeza maboresho ambayo kwenye B yalikuwa ni vikwazo. C ilitengenezwa maalum kwa ajili ya kutengenezea OPERATING SYSTEMS kwa kipindi hicho UNIX. Hata mbunifu wa B alipotengeneza B alianza kuitumia kuandikia UNIX OPERATING SYSTEM. C ilikuwa rahisi sana kutumia, hivyo ikaanza kutumika katika matumizi mengine nje ya OPERATING SYSTEMS. Haikuchukua muda mrefu C ikawa lugha maarufu sana duniani kote ya kuandikia programu za kompyuta. Umaarufu wa C ulichangiwa na urahisi wake, ambapo programmer aliweza kufanya chochote alichotaka kirahisi bila kupitia vikwazo vingi. Vile vile programu za kubadilisha C kwenda kwenye MACHINE CODE yaani COMPILER zilipatik

Jinsi kuprogramu kompyuta kunavyofanya kazi

Je unajiuliza ni namna gani kuprogramu kompyuta kunavyofanya kazi? Leo tutaingia ndani ya kompyuta na kuelewa namna inavyofanya kazi. MACHINE CODE NA ASSEMBLY LANGUAGE Kwanza kabisa inabidi tuelewe kwamba kompyuta inaelewa sifuri na moja au ON na OFF pekee, ambazo huitwa BINARY DIGITS. Mfululizo wa hizi binary digits kwa namna ambayo kompyuta inaelewa huitwa MACHINE CODE yaani lugha ya mashine. Kwa mfano, Kujumlisha kunaweza kuwakilishwa na 1010 kutoa kukawakilishwa na 1011 ufuatao ni mfano wa programu katika MACHINE CODE: 0011 1111 1010 0111 1011 0110 ... na kuendelea sasa huu mfululizo wa haya maelezo (INSTRUCTIONS) ndio unaounda programu ya kompyuta. Lakini kuna tatizo moja ni vigumu sana kuandika programu kwa machine code, yaani kwa sifuri na moja. kutokana na ugumu huu lugha nyingine ambayo ni rahisi kwa mwanadamu iliundwa ambayo ni ASSEMBLY LANGUAGE. Lugha hii inatumia maneno kuwakilisha zile zile binary digits. kwa hivyo badala ya programmer kuandika 1010 anaandika A