Je unajiuliza ni namna gani kuprogramu kompyuta kunavyofanya kazi? Leo tutaingia ndani ya kompyuta na kuelewa namna inavyofanya kazi.
- MACHINE CODE NA ASSEMBLY LANGUAGE
Kwa mfano,
Kujumlisha kunaweza kuwakilishwa na 1010
kutoa kukawakilishwa na 1011
ufuatao ni mfano wa programu katika MACHINE CODE:
0011 1111
1010 0111
1011 0110
... na kuendelea
Lugha hii inatumia maneno kuwakilisha zile zile binary digits. kwa hivyo badala ya programmer kuandika 1010 anaandika ADD, au badala ya kuandika 1011 anaandika SUB.
ufuatao ni mfano wa programu katika ASSEMBLY:
MOV A,7
ADD A,B
SUB A,B
... na kuendelea
- HIGH-LEVEL LANGUAGES
ufuatao ni mfano wa programu katika C:
printf("HAKUNA MATATA!");
Inabidi tukumbuke kuwa lugha asili ya kompyuta ni MACHINE CODE hivyo pamoja na kuandika programu kwa kutumia HIGH-LEVEL LANGUAGE inabidi programu hiyo ibadilishwe kwenda kwenye MACHINE CODE. Ili kubadilisha programu ya C kwenda kwenye MACHINE CODE programu iitwayo COMPILER hutumika.
- HITIMISHO
Comments
Post a Comment