Skip to main content

Posts

Jinsi ya kutumia nginx kama proxy au load balancer

Je una application ambayo inalisten kwenye port fulani na ungependa port isiwepo kwenye url ya hiyo application? Au una nodejs application inayorun kwenye port fulani? kiufupi unataka kubadili https://domain.com:8080/api kuwa https://domain.com/app1/api Katika somo hili tutajifunza namna ya kutumia nginx kama proxy. nginx ni web server maarufu sana, pamoja na umaarufu wake kama web server pia inaweza kutumika kama proxy au load balancer. 1. Basic setup server { listen 80; server_name domain.com www.domain.com; ... location /app1/api { proxy_pass http://localhost:8080; } ... } location /app1/api inaiambia nginx ifananishe path ya url kama imematch /app1/api basi ipitishe request zote kwenda kwenye upstream server iliyopo kwenye url http://localhost:8080. Hii URL inaweza kuwa server nyigine kutegemea application yako ipo wapi. Kwa server nyingine URL inaweza kuwa proxy_pass http://IP_ADDRESS:PORT; 2. HTTP Headers Kwa ka
Recent posts

Control structures katika C

Control Structures katika C Katika somo hili tutajifunza vitu au vipande mbali mbali vinavyounda programu kwa ujumla. Kwa kawaida kompyuta inarun programu mstari mmoja baada ya mwingine kwa kufuatana upi umeanza na upi unafuata. Mstari wa kwanza unarun, kisha unaofuatia na kuendelea hadi mwisho wa programu. Ili kuwepo na wigo mpana wa kuunda programu inabidi tuweze kuhama au kuruka mstari mmoja kwenda mwingine kutegemeana na masharti. Hii huwa inaitwa "Transfer of Control". Hapo awali programmers walikuwa wanatumia goto statement, ambayo inaiambia programu iende kwenye mstari fulani kutegemea na sharti fulani. Ilikuja kugundulika kuwa hii goto statement ilisababisha ugumu mkubwa kwa watengenezaji wa programu kwani kwenye programu kubwa ya kiuhalisia unakuta kuna goto nyingi ambapo inafika kipindi inakua vigumu kujua au kukumbuka statement fulani ilikua kwa sababu gani. Katika utafiti uliofanywa na Bohm na Jacopini walifanikiwa kuonesha kuwa programu zinaweza kutenge

Jinsi ya kuangalia faini za makosa ya barabarani Tanzania

Je ungependa kufahamu namna ya kucheck kama gari yako inadaiwa au haidaiwi? Unaweza kupata taarifa hizi kwa kutumia mtandao kwa wale wenye simu za internet, vile vile unaweza kutumia simu ya kawaida isiyo na internet. Kwa njia ya mtandao Kwa kutumia mtandao tembelea link ifuatayo. http://tms.tpf.go.tz Ukurasa ukifunguka ingiza namba ya gari lako, hapo utaona faini zilizopo katika gari lako. Pia unaweza kuchagua kuingiza namba ya leseni, ili upate faini zilizoandikwa katika leseni yako. Kwa njia ya simu Kwa kutumia simu ya kawaida piga *152*75#  , kisha fuata maelekezo, ukishamaliza utatumiwa ujumbe mfupi wenye taarifa za faini.

Fahamu file aina ya zip na jinsi ya kulitumia

Umewahi kudownload file kwenye internet na kukuta hilo file ni zip na ukashindwa kulifungua? Au umepokea barua pepe ndani yake kumeambatanishwa na file la zip? Au una file kubwa la game au software nyingine unataka kuliweka kwenye DVD lakini halitoshi kwenye hiyo DVD? Katika makala hii tutaangalia kwa undani file la zip (kifurushi) na matumizi yake mbali mbali. File la zip ni nini? File la zip ni file ambalo linakusanya mafile mengine na kuyaweka katika file moja. Hii huwa inarahisa kazi tofauti mfano kutuma barua pepe, badala ya kutuma mafile 10 yaliyomo kwenye folder moja, unaweza kutengeneza zip file moja na kulituma. Pia zip file husaidia kupunguza size ya file. Mfano mzuri wa mafile ambayo hupungua size maradufu ni mafile ya maandishi(text). Mafile ya picha, sauti au video mara nyingi hayapungui size sana kwa sababu aina za hayo mafile tayari yalishajaribu kuyapunguza size. Naandaa vipi file la zip? Ni rahisi sana kutengeneza file la zip, kwani utengenezaji wa file la zi

Matokeo ya kidato cha sita 2018 haya hapa!

Baraza la mitihani Tanzania limetangaza matokeo ya kidato cha sita mwaka 2018. BONYEZA HAPA KWENDA KWENYE MATOKEO! Akizungumza na vyombo vya habari Dkt. Msonde alisema ufaulu kwa ujumla umeongezeka kutoka asilimia 96.06 ya mwaka jana na kuwa asilimia 97.12 mwaka huu, ingawa ufaulu katika masomo ya sayansi umeshuka kulinganisha na masomo ya biashara na sanaa. Vile vile ufaulu katika madaraja ya I, II na III umeongezeka ukilinganisha na mwaka jana. Ufaulu wa madaraja haya umeongezeka kwa asilimia 1.80 kutoka asilimia 93.72 ya mwaka jana na kuwa asilimia 95.52 kwa mwaka huu. Shule kumi zilizofaulu vizuri kitaifa ni kama ifuatavyo Na Shule Idadi ya watahiniwa Mkoa 1 Kibaha 121 Pwani 2 Kisimiri 68 Arusha 3 Kemebos 32 Kagera 4 Mzumbe 121 Morogoro 5 Feza Boys 93 Dar es salaam 6 Marian Boys 78 Pwani 7 Ahmes 76 Pwani 8 St Mary's Mazinde Juu 189 Tanga 9 Marian Girls 71 Pwani 10 Feza Girls 75 Dar es salaam BONY

Jifunze kutype kwenye kompyuta bila kuangalia keyboard

Je unataka kuongeza ufanisi katika kazi zako za kompyuta? Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutype(kuandika) haraka haraka katika keyboard ya kompyuta bila kuangalia. Kutype haraka katika kompyuta ni ujuzi ambao kila mtu anaweza kujifunza japo wengi hudhani wataalamu wa kompyuta ndio wanafanya mambo hayo. Ni ujuzi rahisi sana kama mtu ni mwenye bidii hata ndani ya mwezi unaweza kujifunza. Kuna usemi usemao mti wa kudakia samaki (fishing rod) ni mwendelezo wa mkono wa mvuvi, kwa maana mvuvi mahiri anaweza kuhisi pindi samaki anapokuwa maaneo ya mti wake. Kama fishing rod ilivyo kwa mvuvi, keyboard ya kompyuta inabidi iwe mwendelezo wa vidole vyako ili uwe mtumiaji wa kompyuta mzuri. Katika keyboard ya kompyuta kila kidole kina sehemu yake na kina sehemu kinaweza kwenda. Kujifunza kutype ni kujifunza namna ya kutumia vidole vyako inavyotakiwa. Katika kutype jambo kubwa la kuepuka ni kuinua mkono ili kufuata kitufe fulani, bila shaka kuna wakati utahitaji kuinua mkono lakini hii

Ujue ujanja wa “Fikiria Namba” kihesabu

Je unataka kuwa mjanja wa kusoma fikra za watu? Hapa tutaona namna ya kutumia hesabu kiujanja zaidi. Ni jambo ambalo watu wengi hawalijui hivyo kuwa rahisi kudanganywa na watu wanaojifanya wanasoma akili za watu. Ujanja wa variable mbili( Ujanja wa 10x + y) Katika mfano huu ili usiwe kihesabu zaidi na rahisi kwa kila mtu kuelewa ntatoa mfano wa namna inavyotumika kisha ntawaonyesha kihesabu wewe unavyoweza kufanya na pia kutengeneza mlinganyo wako mwenyewe. Mfano mtu anaweza kuja akakuambia leo ntakutajia kwenu mpo wangapi, watoto wa kiume ni wangapi na wakike ni wangapi. Ataanza kukuambia chukua idadi ya watoto wa kiume zidisha kwa mbili, kisha jibu jumlisha na tatu, jibu lake zidisha na tano, kisha jumlisha idadi ya watoto wa kike, kisha toa 15 katika jibu. Baada ya hapo atakuuliza jibu ni ngapi. Ukimpa jibu tuseme 23, atakuambia mpo watoto watano, wakiume wawili na wakike watatu. Hapo utaona jamaa bonge la superhero!! Ngoja tuone namna yakufanya huu ujanja kihesabu Tuchuk